VIONGOZI MBALIMBALI WATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WINNIE MANDELA


Viongozi mbalimbali na watu mashuhuri wametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Winnie Mandela, aliyekuwa mke wa rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela aliyefariki siku ya jana akiw ana umri wa miaka 81.

Winnie Mandela mkutano mkuu wa ANC 54th ANC Johannesburg.
WINNIE MANDELA

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema Winnie alikuwa mwanamke shupavu na imara katika harakati za ukombozi za Afrika Kusini.

Askofu Mkuu mstaafu wa Afrika Kusini Desmond Tutu, amesema Winnie ni jasiri katika historia ya vizazi vya wanaharakati ambaye alikataa kuwasujudia waliomfunga mumewe.

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika, Moussa Faki Mahamat amesema umoja huo unaungana na bara la Afrika kuomboleza kifo cha Winnie ambaye siku zote atakumbukwa kama mwanaharakati asiye na woga na aliyejitoa maisha yake kwa ajili ya kupigania uhuru wa Afrika Kusini na wanawake wote.

Viongozi wengine waliotoa salama zao za rambirambi ni Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga.

VIONGOZI MBALIMBALI WATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WINNIE MANDELA VIONGOZI MBALIMBALI WATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WINNIE MANDELA Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments