MKUU WA WILAYA YA MOMBA ATAKIWA KUMCHUKULIA HATUA MKANDARASI ANAYESIMAMIA UKARABATI WA KITUO CHA AFYA TUNDUMA.

TAREHE 17-01-2018


Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Dakta Faustine Ndungulile amemwegiza mkuu wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Bw. Juma Ilando kumchukulia hatua za kisheria mkandarasi aliyesimamia ukarabati wa kituo cha afya cha Tunduma kutokana na kushindwa kusimamia mradi huo ipasavyo.

Akitoa maagizo hayo mkoani Songwe Mh Ndugulile amesema kuwa amebaini kuwepo kwa mapungufu mengi katika ukarabati wa kituo hicho ikiwemo mkandarasi huyo kufanya kazi  ya ujenzi bila ramani pamoja na kutumia shilingi milioni mia moja kujenga msingi peke yake jambo ambalo amelitilia mashaka.

Mh Ndugulile ametoa wiki mbili kwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo kutoa taarifa ya mpango kazi wa fedha kiasi cha shilingi milioni mia tano ambazo zilitolewa kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho.


Mkandarasi huyo ambaye ni Bw Sosypeter Msonja anadaiwa kushindwa kusimamia ukarabati wa kituo cha afya cha mji mdogo wa Tunduma ambapo serikali ilitoa kiasi cha shilingi miloni mia tano kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti chumba cha upasuaji pamoja na nyumba ya mtumishi .
MKUU WA WILAYA YA MOMBA ATAKIWA KUMCHUKULIA HATUA MKANDARASI ANAYESIMAMIA UKARABATI WA KITUO CHA AFYA TUNDUMA. MKUU WA WILAYA YA MOMBA ATAKIWA KUMCHUKULIA HATUA MKANDARASI ANAYESIMAMIA UKARABATI WA KITUO CHA AFYA TUNDUMA. Reviewed by safina radio on January 17, 2018 Rating: 5

No comments