WATU 37 WAFARIKI KATIKA MAFURIKO NCHINI DRC CONGO.
TAREHE 05-01-2017

Maafisa wa serikali ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo wamesema watu zaidi ya 37 wamefariki baada ya mafuriko
kuukumba mji mkuu wa wa nchi hiyo Kinshasa, kufuatia mvua kubwa.

Waziri wa jimbo
anayeangazia masuala ya kiafya na kijamii Dominique Weloli amesema wengi wa waliofariki ni wakazi wa
mitaa ya mabanda ambapo nyumba nyingi zimeharibiwa na maji ya mafuriko na
maporomo ya ardhi.
Kati ya wakazi milioni kumi wa mji wa Kinshasa
huishi katika makazi duni katika maeneo tambarare na yenye miundo mbinu duni ya kuondoa maji taka .
Hata
hivyo kumekuwa na matukio ya vifo vinavyotokana na mafuriko karibu kila mwaka wakati
wa msimu wa mvua kubwa nchini humo.
WATU 37 WAFARIKI KATIKA MAFURIKO NCHINI DRC CONGO.
Reviewed by safina radio
on
January 05, 2018
Rating:
No comments