WAANDAMANAJI SITA NCHINI DRC WAUAWA.

TAREHE 22-01-2018
Polisi nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Congo wakitawanya waandamanaji
Image caption
Waandamanaji sita wameuawa katika nchi ya  Jamhuri ya Demokrasia ya Congo kufuatia makabiliano na polisi waliokuwa wakizima maandamano yanayoendelea kusambaa nchini humo kumshinikiza rais Joseph Kabila kuondoka madarakani.
Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji mjini Kinshasa,ambapo maandamano kama hayo pia yanaendelea katika miji mingine ndani ya taifa hilo.
Msemaji wa umoja wa mataifa nchini Jamhuri ya Congo amesema kuwa Zaidi ya watu 50 walijeruhiwa siku ya jumapili.
Waziri wa zamani Jean Baptise Sondji ameliambia shirika la habari la AFP kwamba alishuhudia mauaji ya mtoto mwenye umri wa miaka 16 nje ya kanisa eneo la Kitambo mjini Kinshasa.

Serikali ya Congo imepiga marufuku maandamano ya aina yoyote huku siku  ya jumamosi mawasiliano ya internet yalikatwa mjini Kinshasa.
WAANDAMANAJI SITA NCHINI DRC WAUAWA. WAANDAMANAJI SITA NCHINI DRC  WAUAWA. Reviewed by safina radio on January 22, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.