MAUTI INAYOSHIKILIA MALANGO YA MIGUU YA WATU HUFANYA KUSHINDWA KUFANIKIWA KIMAISHA.


ARUSHA

12 February, 2018.
Waumini wakiwa wamezama katika maombi ya kina katika huduma ya maombi ya radio safina.

Jamii imetakiwa kushughulikia roho ya mauti inayoshikilia malango ya miguu ya watu na kuwafanya kushindwa kufanikiwa kimaisha huku wengine wakikabiliwa na magonjwa sugu na vifo.  

Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi mchana imekuandalia maombi maalumu ya mwendelezo wa kushughulikia kiapo cha mauti kwenye eneo la malango ya miguu kiroho na kimwili.

Aidha kwa mujibu wa somo hilo imebainika kuwa wako watu ambao miguu yao imebeba mauti badala ya amani au hali ambayo inasababisha wao kusongwa na matizo malimbali kama vile kutokufanikiwa kielimu kiuchumi kiafya na kifamilia kwa ujumla

Pia upo  uwezekano wa ndoa kukamatwa na roho ya mauti na mara nyingine kuwafanya kukosa watoto,kuwa na migogoro isiyoisha, umasikini uliokithiri, ambapo jamii imeshauriwa kufahamu kuwa  njia pekee ya kuondokana na roho hiyo ya mauti  ni kwenda mbele za Mungu kwa maombi.

Hata hivyo maombi hayo ya kesho yataambatana na kitendo cha imani cha kuosha miguu na maji ambayo tayari yameshaombewa kwa kusudi la kufungua miguu ya watu iliyoshikiliwa kwenye malango ya mauti.

MAUTI INAYOSHIKILIA MALANGO YA MIGUU YA WATU HUFANYA KUSHINDWA KUFANIKIWA KIMAISHA. MAUTI INAYOSHIKILIA MALANGO YA MIGUU YA WATU HUFANYA KUSHINDWA KUFANIKIWA KIMAISHA. Reviewed by safina radio on February 12, 2018 Rating: 5

No comments