Shirika linalofuatilia masuala ya haki za kibinadamu nchini Syria limesema, mashambulizi mapya ambayo yamefanywa na vikosi vya Syria leo katika eneo linaloshikiliwa na waasi katika eneo la Ghouta Mashariki, yamesababisha vifo vya raia 10, huku watu 9 miongoni mwao wakiwa wa familia moja.
DAMASCUSS.
Shirika linalofuatilia masuala ya haki za kibinadamu
nchini Syria limesema, mashambulizi mapya ambayo yamefanywa na vikosi vya Syria
leo katika eneo linaloshikiliwa na waasi katika eneo la Ghouta Mashariki,
yamesababisha vifo vya raia 10, huku watu 9 miongoni mwao wakiwa wa familia
moja.
Shirika hilo limeongeza kwa kusema kuwa mashambulizi
ya angani katika mji wa Douma ambao ndio mji mkuu Ghouta Mashariki yameharibu
majengo na kuwazika watu wakiwa hai.
Hayo yanajiri huku wanaharakati pamoja na kundi la
uangalizi la haki za binadamu wakisema kuwa shambulizi linaloshukiwa kuwa la
kemikali inayoaminiwa kuwa gesi ya chlorine ambalo limefanywa katika eneo la Ghouta
Mashariki, limemuua mtoto mmoja.
Watu 14 pia walikumbwa na matatizo ya kupumua baada
ya ndege ya kivita ya Syria kushambulia kijiji cha al-Shofa niyeh.
Shirika linalofuatilia masuala ya haki za kibinadamu nchini Syria limesema, mashambulizi mapya ambayo yamefanywa na vikosi vya Syria leo katika eneo linaloshikiliwa na waasi katika eneo la Ghouta Mashariki, yamesababisha vifo vya raia 10, huku watu 9 miongoni mwao wakiwa wa familia moja.
Reviewed by safina radio
on
February 26, 2018
Rating:

No comments