NAIBU WAZIRI NYONGO ASEMA KUWA SERIKALI IMEJIPANGA KUDHIBITI MIANYA YOTE YA UTOROSHWAJI WA MADINI .


ARUSHA.



Naibu waziri wa madini Stanislaus Nyongo amesema kuwa serikali imejipanga kudhibiti mianya y
ote ya utoroshwaji wa madini hususani madini ya Tanzanite na ubadhilifu unaoendelea katika madini hayo ili kufanya sekta ya madini inufaishe taifa pamoja na wananchi kwa ujumla.

Mh Nyongo ameyasema hayo wakati akizungumza na wafanyabiashara na wachimbaji wa madini kutoka Mikoa ya Manyara na Arusha kwenye kikao cha kusikiliza changamoto zinazowakabili wanyabiashara na wachimbaji hao kilichofanyika katika ofisi za madini Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha.

 Amesema kuwa serikali haifurahii  kuona wafanyabiashara na wachimbaji wa madini wakiumia bali  inataka  kuweka utaratibu mzuri utakaofanya madini hayo  kuwa na manufaa kwa taifa na kueleza kuwa mpaka sasa mapato yatokanayo na sekta ya madini hayaridhishi kwani faida yake  ni asilimia 04.2 pekee.

Kwa upande wake Naibu waziri mwenza wa madini Dotto  Biteko amesema kuwa lengo la Rais John Magufuli ni kuona madini hayo yanawanufaisha wananchi wote na kuahidi kuwa watafanya kila linalowezekana kuhakikisha wafanyabiashara na wachimbaji hao wanatoka katika changamoto hiyo na kuwezesha kupanda kwa uchumi wa nchi kupitia sekta ya madini.

Naye Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara na wachimbaji wa madini (TAMIDA) Sammy Mollel ameeleza kuwa wao kama wafanyabiashara hawataki madini yatoroshwe  hivyo ni vyema  serikali ikae  nao ili kuweze kujua ni njia gani watatumia katika kuondokana na changamoto hiyo inayofanya hali ya biashara ya madini kuwa mbaya.

NAIBU WAZIRI NYONGO ASEMA KUWA SERIKALI IMEJIPANGA KUDHIBITI MIANYA YOTE YA UTOROSHWAJI WA MADINI . NAIBU WAZIRI NYONGO ASEMA KUWA SERIKALI IMEJIPANGA KUDHIBITI MIANYA YOTE YA UTOROSHWAJI WA MADINI . Reviewed by safina radio on February 15, 2018 Rating: 5

No comments