JAFFO ATOA MAAGIZO KWA MAMLAKA ZA MIJI, WILAYA, NA MIJI MIDOGO KUFUNGA DIRA ZA MAJI KWA ASILIMIA 90.


DODOMA.


Taarifa ya Habari 01:00 mchana, 15 February, 2018.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI Mh Seleman Jaffo ametoa maagizo kwa mamlaka za miji, wilaya na miji midogo kufunga dira za maji kwa asilimia 90 hadi ifikapo mwezi Juni mwaka huu.

Mh Jaffo ametoa maagizo hayo mjini Dodoma katika mkutano wa uzinduzi wa ripoti ya utendaji wa mamlaka za maji za miji, wilaya na miji midogo ulioandaliwa na mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati EWURA.

Aidha, Jaffo amesema kuwa katika kipindi cha miaka tisa (9) mfululizo cha kutoa ripoti ya utekelezaji wa mamlaka za maji nchini haiwezekani kuona kuwa bado kuna mamlaka ambazo hazijafunga dira za maji kwa wateja wao.

Hata hivyo, amesema baada ya kipindi cha miezi sita kupita kama bado kutakuwepo na mamlaka ya maji ambayo haijafunga dira ya maji atavunja bodi  ya mamlaka hiyo na kumfukuza kazi meneja husika.

JAFFO ATOA MAAGIZO KWA MAMLAKA ZA MIJI, WILAYA, NA MIJI MIDOGO KUFUNGA DIRA ZA MAJI KWA ASILIMIA 90. JAFFO ATOA MAAGIZO KWA MAMLAKA ZA MIJI, WILAYA, NA MIJI MIDOGO KUFUNGA DIRA ZA MAJI KWA ASILIMIA 90. Reviewed by safina radio on February 15, 2018 Rating: 5

No comments