MARTIN SCHULZ ATANGAZA KUJIUZULU NAFASI YAKE KAMA KIONGOZI WA CHAMA HICHO.


BERLIN.

Taarifa ya Habari saa 01:00 mchana, 14 February, 2018.

Martin Schulz, Kiongozi wa chama cha Social Democratic, SPD.

Kiongozi wa chama cha Social Democratic, SPD Martin Schulz ametangaza kujiuzulu mara moja nafasi yake kama kiongozi wa chama hicho.

 Schulz, aliyeshindwa kwenye kinyang'anyiro cha ukansela na kiongozi wa zamani wa Umoja wa Ulaya alichukua uamuzi wa kujiuzulu baada ya siku kadhaa za mjadala wa wanachama wa SPD.

Waziri wa zamani wa ajira na kiongozi wa sasa wa wabunge wa SPD, Andrea Nahles alichaguliwa kuchukua nafasi yake katika maamuzi ya pamoja ya viongozi wa SPD.

Iwapo atachaguliwa katika mkutano utakaofanyika katika mji wa Wiesbaden mwezi Aprili, Nahles atakuwa mwanamke wa kwanza kuongoza, katika historia ya miaka 150 ya chama hicho.

Kulingana na duru za ndani ya SPD Meya wa Hamburg Olaf Scholz, anayetarajiwa kuwa waziri wa fedha, atakiongoza chama hicho hadi kitakapofanya mkutano wake Aprili 22.

MARTIN SCHULZ ATANGAZA KUJIUZULU NAFASI YAKE KAMA KIONGOZI WA CHAMA HICHO. MARTIN SCHULZ ATANGAZA KUJIUZULU NAFASI YAKE KAMA KIONGOZI WA CHAMA HICHO. Reviewed by safina radio on February 14, 2018 Rating: 5

No comments