NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA MH. KANGI LUGOLA AWATAKA WAWEKEZAJI KUFUATA SHERIA.


TAREHE 13-02-2018
MH.LUGOLA  KUSHOTO 


Naibu waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira Mh Kangi Lugola amewataka wawekezaji wadogo na wakubwa kufuata sheria na kanuni na mazingira pamoja na matumizi sahihi ya ardhi ili kulinda afya za wakazi wa maeneo hayo hapa nchini.

Mh Lugola ametoa wito huo wakati wa ziara yake ya kuzuri kiwanda kidogo kilichopo eneo la Mwangati jijini Dar-es-salaam,baada ya kupokea malalamiko kuwa kiwanda hicho kipo eneo la makazi ya watu na kinafanya uchafuzi wa mazingira.

Naye meneja wa kiwanda hicho kinacholalamikiwa cha Nethin Company Limited Bw Atuman Ramadhan amesema kuwa amepokea maagizo ya naibu waziri huyo na watayafanyia kazi.

Kwa upande wake mbunge wa Ukonga Mh Mwita Waitara ameshukuru mwitikio wa naibu waziri huyo kufika katika kiwanda kinacholalamikiwa na wananchi na kukitolea maelekezo.

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA MH. KANGI LUGOLA AWATAKA WAWEKEZAJI KUFUATA SHERIA. NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA  MH. KANGI LUGOLA AWATAKA WAWEKEZAJI KUFUATA SHERIA. Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments