JAMII IKISIMAMA VYEMA KATIKA MAOMBI YA UKOMBOZI KWA NJIA YA TOBA NA REHEMA KATIKA ENEO LA NDOA NA MAHUSIANO MUNGU ATACHUKUA NAFASI NA VILIO VYA NDOA, UCHUMI NA AFYA VITAKOMA.



ARUSHA

Imebainishwa kuwa endapo jamii itasimama imara katika maombi ya ukombozi kwa njia ya Toba na Rehema katika eneo la ndoa na mahusiano, vilio vya ndoa, uchumi na afya  vitaisha kutokana na Mungu kuchukuwa nafasi.

Toba na Rehema.

Huduma ya redio safina kesho kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana katika ukumbi wa maombi ulioko mbauda jijini Arusha imekuandalia maombi maalumu ya kushughulikia mauti katika ndoa na uchumba ambayo imeonekana kuwatesa watu wengi katika jamii.

Huduma ya redio safina.
Aidha kutokana na watu wengi kuendelea kutaabika katika eneo la ndoa na uchumba imebainika kuwa njia pekee ya kukabiliana na matatizo hayo ni watu kujikita kwenye maombi ya ukombozi kwa kuomba toba na rehema mbele za  Mungu ili aweze kusamehe na kuondoa roho hizo zinazowatesa vijana kwenye eneo la uchumba pamoja na wanandoa.

Roho zinazowatesa vijana kwenye eneo la uchumba pamoja na wanandoa.

Aidha kesho katika ukumbi wa safina redio watumishi watashughulikia nguvu ya roho ya mauti ndani ya ndoa katika maeneo tofauti kama vile mauti ya maneno,mauti iliyofanywa kwa vitendo,pamoja na mauti iliyosababishwa kwa njia za uganga na uchawi ili kuwadhibiti wanandoa kiuchumi pamoja na vijana kutokuingia kwenye mahusiano kwa wakati.
Shughulikia nguvu ya roho ya mauti ndani ya ndoa katika maeneo tofauti.
Pamoja na hayo watu mbalimbali wataombewa ili kufunguliwa kwenye vifungo vinavyowatesa wakiwemo wagonjwa na watu wasiokuwa na ajira kutokana na kudhibitiwa na roho ya mauti.


JAMII IKISIMAMA VYEMA KATIKA MAOMBI YA UKOMBOZI KWA NJIA YA TOBA NA REHEMA KATIKA ENEO LA NDOA NA MAHUSIANO MUNGU ATACHUKUA NAFASI NA VILIO VYA NDOA, UCHUMI NA AFYA VITAKOMA. JAMII IKISIMAMA VYEMA KATIKA MAOMBI YA UKOMBOZI KWA NJIA YA TOBA NA REHEMA KATIKA ENEO LA NDOA NA MAHUSIANO MUNGU ATACHUKUA NAFASI NA VILIO VYA NDOA, UCHUMI NA AFYA VITAKOMA. Reviewed by safina radio on February 28, 2018 Rating: 5

No comments