Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa amesema kuwa serikali haitamvumilia mtu yeyote yule atakayekatisha ndoto za mtoto wa kike kwa kumpa ujauzito.
MTWARA.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh
Majaliwa Kassim Majaliwa amesema kuwa serikali haitamvumilia mtu yeyote yule
atakayekatisha ndoto za mtoto wa kike kwa kumpa ujauzito.
![]() |
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa |
Mh Majaliwa ameyasema hayo leo wakati akiendelea na ziara
yake ya siku tatu mkoani Mtwara,ambapo amesema kuwa watoto wa kike wanatakiwa
kuthaminiwa katika jamii na kuwezeshwa ili waweze kuendelea na masomo bila
kubugudhiwa na atakayebainika kumpa mtoto wa kike ujauzito atachukuliwa hatua
kali za kisheria.
Amesema kuwa serikali itatoa adhabu kali ya kifungo
cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike kwa kumpa
ujauzito pamoja na kumchukulia hatua kali za kisheria mzazi au mlezi
atakayeshiriki kumkwamisha mtoto wa kike kumaliza masomo yake.
Hata hivyo waziri mkuu yupo katika ziara ya siku
tatu mkoani Mtwara kiwa anaendelea na zoezi la kukagua miradi pamoja na kutatua
changamoto mbalimbali zzinazowakabili wananchi.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa amesema kuwa serikali haitamvumilia mtu yeyote yule atakayekatisha ndoto za mtoto wa kike kwa kumpa ujauzito.
Reviewed by safina radio
on
February 27, 2018
Rating:

No comments