RAMAPHOSA AAPISHWA KUWA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI.


JOHANESBURGE.


Cyril Ramaphosa.


Mwenyekiti wa chama tawala cha ANC Cyril Ramaphosa ameapishwa kuwa rais wa Afrika Kusini baada ya rais wa taifa hilo Jacob Zuma kujiuzulu.

Rais huyo mpya alikuwa mtu wa pekee aliyeteuliwa leo huku uteuzi huo ukiungwa mkono kwa shangwe bungeni.

Bwana Zuma alikuwa chini ya shinikizo kali kutoka kwa chama chake cha ANC kilichomtaka ajiuzulu la sivyo akabiliwe na kura ya kutokuwa na imani dhidi yake bungeni.

Katika taarifa ya runinga, alisema kuwa anajiuzulu mara moja lakini hakubaliani na uamuzi wa chama,ambapo anakabiliwa na madai kadhaa ya ufisadi lakini amekana kufanya makosa yoyote.

RAMAPHOSA AAPISHWA KUWA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI. RAMAPHOSA AAPISHWA KUWA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI. Reviewed by safina radio on February 15, 2018 Rating: 5

No comments