WAZIRI MKUU WA JAPANI SHINZO ABE AMESEMA KUWA USHIRIKIANO WAKE NA MAREKANI NA KOREA KUSINI NI IMARA

TAREHE 09-02-2018

Image result for PICHA YA WAZIRI MKUU WA JAPAN SHINZO ABE


Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe, leo amesema kuwa anataka kutuma ujumbe duniani kwamba ushirikiano kati ya Marekani, Japan na Korea Kusini kuhusu kitisho cha Korea Kaskazini bado ni imara.

Abe, ambaye anatarajiwa kukutana baadaye leo na Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in, amesema kabla ya kwenda Pyeongchang katika ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya msimu wa baridi, kuwa yeye na Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence wamesisitiza kuwa nchi hizo mbili zimesimama pamoja kwa asilimia mia moja.

Hapo jana, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un aliongoza maonesho ya kijeshi ambapo maelfu ya wanajeshi na vifaru waliandaa gwaride, kuadhimisha miongo saba tangu kuundwa kwa jeshi la nchi hiyo.

Gwaride la kijeshi la Korea Kaskazini liliandaliwa mara ya mwisho Aprili 2017, na kuoneshwa moja kwa moja kwenye televisheni.

Korea Kaskazini inaitumia michezo ya Olimpiki ya Pyeongchang inayoandaliwa Korea Kusini ili kuanzisha urafiki, ikiwa ni pamoja na kuwatuma watumbuizaji, makundi ya washangiliaji na dadake Kim Jong Un katika michezo hiyo.

WAZIRI MKUU WA JAPANI SHINZO ABE AMESEMA KUWA USHIRIKIANO WAKE NA MAREKANI NA KOREA KUSINI NI IMARA WAZIRI MKUU  WA JAPANI SHINZO ABE AMESEMA KUWA USHIRIKIANO WAKE NA MAREKANI  NA KOREA KUSINI NI IMARA Reviewed by safina radio on February 09, 2018 Rating: 5

No comments