KIHAMIA, BILIONI 6.9 ZATENGWA KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI.



ARUSHA.

Taarifa ya habari saa 08:00 usiku, 13 February, 2018.
Bw Athumani Kihamia Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Arusha

Jumla ya Fedha shilingi bilioni 6.9 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kuwahudumia wananchi hususani katika sekta ya elimu,afya na miundombinu ya barabara.

Hayo yameyasemwa Bw Athumani Kihamia Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Arusha katika kikao maalum cha Kamati ya Maendeleo ya Wilaya kupitia utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17 na bajeti mpya ya halmashauri ya jiji la Arusha kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambacho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali.

Kihamia amesema kuwa vikao vya mapendekezo ya bajeti na watendaji wa kata,viongozi wa dini,makundi ya wazee na vijana tayari vimeshaanza ili kupata maoni yao yatakayo wawezesha katika kutatua changamoto za wananchi iwapo zitatekelezwa kama walivyopanga.

Aidha amesema kutokana na ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza baadhi ya wajumbe wamependekeza kuwekwa kwa kipaumbele cha ujenzi wa madarasa ili kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani jambo ambalo litasaidia kuboresha maendeleo ya taaluma shuleni.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Dakaro ameitaka Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa inajenga madarasa yaliyobaki yapatayo 771 ambayo yatagharimu kiasi cha fedha shilingi  bilioni 4.4 ifikapo mwezi Novemba mwaka huu hadi kukamilika ili kuweza kutatua changamoto ya uhaba wa madarasa uliopo kwa sasa.

Kwaupande wake Naibu Meya wa Jiji la Arusha Viola Lazaro amesema kuwa hulka ya baadhi ya watendaji kushughulikia tatizo la uhaba wa madarasa na kipindi ambacho kina idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga na masomo ya sekondari kimekuwa kikiwagharimu watoto kushindwa kufanya vizuri kitaaluma kutokana na msongamano wa wanafunzi uliopo.

KIHAMIA, BILIONI 6.9 ZATENGWA KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI. KIHAMIA, BILIONI 6.9 ZATENGWA KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI. Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments