Waziri wa elimu sayansi na teknolojia na mafunzo ya ufundi Prf. Joyce Ndalichako amekitaka Chuo Kikuu cha Maount Meru cha jijini Arusha kuacha utaratibu wa kutoa alama za makisio kwa wanafunzi kwani serikali haitasita kukifunga chuo hicho kutokana na utaratibu huo.
ARUSHA.
Waziri wa elimu sayansi na teknolojia na mafunzo ya
ufundi Prf. Joyce Ndalichako amekitaka Chuo Kikuu cha Maount Meru cha jijini
Arusha kuacha utaratibu wa kutoa alama za makisio kwa wanafunzi kwani serikali
haitasita kukifunga chuo hicho kutokana na utaratibu huo.
![]() |
Waziri wa elimu sayansi na teknolojia na mafunzo ya ufundi Prf. Joyce Ndalichako. |
Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo mara baada ya
kutembelea chuo hicho na kuona namna kinavyosimamia utoaji wa elimu ya juu na
kuongeza kuwa wizara yake imeshatoa maagizo kupitia Tume ya Vyuo Vikuu nchini
kuwaondoa wahadhiri ambao hawana sifa za kufundisha lakini agizo hilo mpaka
sasa halijatekelezwa.
Aidha, Waziri Ndalichako amesema kuwa ili wanafunzi
hao waweze kutambulika na kuweza kuajiriwa ndani ya Tanzania inatakiwa mitihani
yao isahihishwe au kuangiliwa na watu wa nje ili alama za matokeo hayo
yatumike.
Pia, Waziri ndalichako ameongeza kuwa endapo suala
hilo halitawezekana, wanafunzi hao wanatakiwa kufanya mtihani na kusahihishwa
ili kuondokana na tatizo hilo la kukisia alama za matokeo pamoja na kuondoa
suala hilo kwa lengo la kutokuharibu mfumo wa elimu ya Tanzania.
Kwa upande, wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mount
Meru Dk. Masau Kituka ameeleza kasoro zilizojitokeza katika matokeo ya wanafunzi
kuwa ni makosa ya walimu na si wanafunzi.
Hata hivyo, udahili wa wanafunzi katika chuo hicho
cha Mount Meru mpaka sasa umesitishwa hadi kitakapo rekebisha kasoro zilizopo.
Waziri wa elimu sayansi na teknolojia na mafunzo ya ufundi Prf. Joyce Ndalichako amekitaka Chuo Kikuu cha Maount Meru cha jijini Arusha kuacha utaratibu wa kutoa alama za makisio kwa wanafunzi kwani serikali haitasita kukifunga chuo hicho kutokana na utaratibu huo.
Reviewed by safina radio
on
February 26, 2018
Rating:

No comments