KAMISHNA MUSLIM, ASKARI WENYE TOCHI MAALUMU WATAKUWAPO KILA KILOMITA MOJA KATIKA ENEO LA KIBUKU.


TANGA.




Polisi kitengo cha usalama barabarani kimesema kuwa kila kilometa moja eneo la Kabuku ilipotokea ajali ya watu watano itakuwa na askari wenye tochi maalumu na watafanya hivyo baada ya kubaini kuwa eneo hilo ni eneo korofi.



Mkuu wa operesheni,Kikosi cha usalama barabarani nchini Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Fortunatus Muslim ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea eneo la Kibuku kuona namna ajali zinavyoweza kudhibitiwa .

Aidha, Kamanda Muslim amesema kuwa katika kipindi cha miezi miwili Januari hadi sasa ajali mbili zimetokea eneo la Kabuku wilayani Handeni mkoani Tanga na kugharimu maisha ya watu kumi na wengine kadhaa kuijeruhiwa.

Amesema amefika katika eneo hilo ili kuona kilichotokea na kuweza kukagua eneo la tukio ambapo tukio hilo lilitokea tarehe 21 mwezi Januari mwaka huu iliyohusisha ajali ya Noah hivyo kutokana na matukio hayo katika eneo hilo linaonesha eneo hilo kuwa ni hatarishi.

Hata hivyo, mapema wiki hii ajali za barabarani katika eneo hilo la Kibuku limesababisha vifo vya watu watano na wengine sita kujeruhiwa.

KAMISHNA MUSLIM, ASKARI WENYE TOCHI MAALUMU WATAKUWAPO KILA KILOMITA MOJA KATIKA ENEO LA KIBUKU. KAMISHNA MUSLIM, ASKARI WENYE TOCHI MAALUMU WATAKUWAPO KILA KILOMITA MOJA KATIKA ENEO LA KIBUKU. Reviewed by safina radio on February 15, 2018 Rating: 5

No comments