UNHCR IMESEMA MIONGONI MWA WATU 11 WALIOUAWA NCHINI RWANDA WATANO NI WAKIMBIZI KUTOKA CONGO.


TAREHE 27-02-2018

BAADHI YA ASKARI WA KULINDA USALAMA
Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limesema miongoni mwa watu 11 waliouliwa Alhamis iliyopita nchini Rwanda, watano walikuwa ni wakimbizi kutoka Congo.

Afisa wa shirika hilo Daniela Lonita amesema vifo hivyo vilitokea katika kambi ya wakimbizi ya Kiziba pamoja na  mji wa karibu wa Kibuye magharibi mwa Rwanda.

Maelfu ya watu walikuwa wamekwenda kuandamana katika ofisi za Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa, baada ya shirika hilo kupunguza ugawaji wa chakula kwa asilimia 10 mwezi Novemba na kwa asilimia 25 kuanzia Januari.

Polisi ya Rwanda imethibitisha vifo vya watu watano pekee katika taarifa yake ya Ijumaa iliopita iliosema kwamba ilichukua hatua baada ya waandamanaji kuwajeruhi maafisa wa polisi saba kwa kutumia mawe, viboko na vyuma.

Hata hivyo Umoja wa Mataifa unaisisitiza serikali ya Rwanda kulifanyia uchunguzi tukio hilo.

UNHCR IMESEMA MIONGONI MWA WATU 11 WALIOUAWA NCHINI RWANDA WATANO NI WAKIMBIZI KUTOKA CONGO. UNHCR IMESEMA MIONGONI MWA WATU 11 WALIOUAWA NCHINI RWANDA WATANO NI WAKIMBIZI KUTOKA CONGO. Reviewed by safina radio on February 27, 2018 Rating: 5

No comments