MAKAMU RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSAN AKIZINDUA MRADI WA REGRO.
IRINGA.
12 February, 2018.
![]() |
Makamu wa Rais wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassani akiwa Iringa kwaziara ya kuzindua miradi mbali mbali ya maendeleo. |
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama
Samia Suluhu Hassan hii leo amezindua mradi wa kuimarisha Usimamizi wa
Maliasili na Kuendeleza Utalii Kanda ya Kusini mwa Tanzania ujulikanao kama
REGRO.
Mh. Samia amezindua mradi huo ikiwa ni siku yake ya nne
ya Ziara ya kikazi mkoani Iringa ambapo amesema kuwa serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania imepokea jumla ya fedha kiasi cha dola milioni 150 kutoka
Benki Kuu ya Dunia kwa ajili ya kutekeleza mradi wa miaka sita.
Aidha, Amesema kuwa lengo la mradi huo ni kukuza utalii
na kipato cha wananchi kwa kuboresha miundombinu, kujenga uwezo katika
usimamizi wa maliasili na kuwezesha wananchi wanaozunguka hifadhi kuzalisha kwa
tija.
Pia amewaasa watendaji wa Taasisi zitakazotekeleza mradi
huo kuwa waadilifu kusimamia mradi huo mkubwa ili kufikia malengo
yanayotarajiwa kwa kuwa mkopo huo utalipwa na watanzania wote hivyo
amewakumbusha kutumia fedha hizo katika shughuli zilizokusudiwa.
Wakati huo huo, Mh Samia amekutana na kuzungumza na
wananchi wa manispaa ya Iringa ambapo amesema kilimo cha korosho ni fursa
nyingine ya kukuza kipato na ni zao linalofanya vizuri kwa sasa huku mikoa ya
Dodoma, Morogoro ikichangamkia kulima zao hilo hivyo amewaasa wananchi
wanaopakana na Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma waanze kulima zao hilo.
Hata hivyo, amesema
kuwa huduma za afya,maji na umeme zitaendelea kuboreshwa ambapo amewataka
wananchi kukataa maambukizi ya virusi vya UKIMWI huku akiwaagiza watendaji wa
serikali kuendelea kuimarisha utawala bora, miundombinu ya reli na barabara.
MAKAMU RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSAN AKIZINDUA MRADI WA REGRO.
Reviewed by safina radio
on
February 12, 2018
Rating:

No comments