Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amewataka wataalamu wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Lindi LUWASA kukaa Kwenye kituo cha kusukuma maji kilichopo kwenye mradi wa maji wa Ng`apa ili kukabiliana na changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara na kusababisha wananchi wa mji wa Lindi kukosa maji.
LINDI.
Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack
Kamwelwe amewataka wataalamu wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Lindi LUWASA
kukaa Kwenye kituo cha kusukuma maji kilichopo kwenye mradi wa maji wa Ng`apa
ili kukabiliana na changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara na
kusababisha wananchi wa mji wa Lindi kukosa maji.
![]() |
Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe. |
Mhandisi Kamwelwe ameyasema hayo alipotembelea mradi
wa maji wa Ng’apa
na kubaini tatizo la umeme linalowasababisha wananchi wa mji huo kukosa maji
mara kwa mara.
Amesema kuwa katika eneo hilo umeme unakuja usiku na
kusababisha bomba hilo la maji kufumuka zaidi ya mara tatu jambo ambalo si la
kawaida ikilinganishwa na maeneo mengine ya Ruvu juu na Ruvu chini mkoani
Pwani.
Hata hivyo mradi wa maji wa Ng’apa unahudumia zaidi
ya wakazi elfu themanini na tano katika mji wa Lindi ambapo waziri huyo
amabaini tatizo la umeme kukatika mara kwa mara na wakati mwingine kutokuwepo
nyakati za usiku na kukosekana kwa mtu wa kuwasha pampu za kusukuma maji hali
inayosababisha kero kubwa kwa wakazi wa mji huo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Lindi Bw Shaibu
Ndamanga ameishukuru serikali kwa uamuzi wake wa kubeba jukumu la kugharamia
umeme kwenye mradi huo na hiyo itasaidi kuondoa tatizo la umeme katika kituo hicho.
Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amewataka wataalamu wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Lindi LUWASA kukaa Kwenye kituo cha kusukuma maji kilichopo kwenye mradi wa maji wa Ng`apa ili kukabiliana na changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara na kusababisha wananchi wa mji wa Lindi kukosa maji.
Reviewed by safina radio
on
February 27, 2018
Rating:

No comments