SERIKALI ITACHUKUA HATUA YA KUIMARISHA MAHAKAMA KWA LENGO LA KUTOA HAKI KWA WANANCHI KWA WAKATI, DK. ALLY MOHAMED SHEIN.
ZANZIBAR.
12 February, 2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Ally Mohamed Shein katika sherehe ya siku ya sheria Zanzibar. |
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa
baraza la mapinduzi Dr Ally Mohamed Shein amesema kuwa serikali itachukua hatua
ya kuimarisha mahakama kwa lengo la kutoa haki kwa wananchi kwa wakati.
Dr Sheikn ametoa kauli hiyo wakati
akizungiumza katika siku ya sheria Zanzibar katika ukumbi wa zamani wa
baraza la wawakilishi Kikwajuni Visiwani
Zanzibar, ambapo amesema kuwa wananchi wanajenga imani na serikali iwapo misngi
ya sheria itafuatwa na mahakama na kuwa huru bila kuingiliwa katika utendaji
wake.
Ameongeza kuwa utawala wa sheria ndio
dira ya mafanikio wa mpango mkuu wa serikali katika kuwaletea wanachi maendeleo
katika sekta zote za kiuchumi na kijamii pamoja na kudumisha amani na utulivu.
Amefafanua kuwa utaratibu huo
utawezesha Zanzibar kutekeleza mpango wa kuimarisha viwanda,utalii,kuvutia
wawekezaji,mfumo mzuri wa kibiashara,kuendeleza kilimo,uvuvi na ufugaji wa
kisasa pamoja na uhifadhi wa mazingira.
Hata hivyo Dr Shekn ameitaka mahakama
kutumia mfumo wa TEHEMA ili kuongeza
ufanisi na tija katika mfumo wa utatuzi wa migogoro na kesi nyingine
mbalimbali.
SERIKALI ITACHUKUA HATUA YA KUIMARISHA MAHAKAMA KWA LENGO LA KUTOA HAKI KWA WANANCHI KWA WAKATI, DK. ALLY MOHAMED SHEIN.
Reviewed by safina radio
on
February 12, 2018
Rating:
No comments