WAZIRI JAFO ATOA RAI KWA JAMII NCHINI KUUNGA MKONO MPANGO WA SERIKALI WA ELIMU BURE


TAREHE 08-02-2018


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI Mh. Dk. Suleman Jaffo ametoa rai kwa jamii nchini kuunga mkono mpango wa serikali wa kutoa elimu bure kwa kujitolea vifaa vya kujifunzia ili kuwawezesha wanafunzi wanaotoka katika familia zenye uhitaji kupata elimu bora.

Waziri Jaffo ametoa rai hiyo wakati wa uzinduzi wa mpango wa kusaidia vifaa vya kijifunzia kwa watoto wanaotoka katika familia zisizo na uwezo uliofanyika katika shule ya msingi ya Ukuzi wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Waziri Jaffo ameeleza kuwa kutokana na ukosefu wa fursa ya vitendea kazi hivyo vya elimu kwa watoto wanaotoka katika familia zenye uhitaji, jamii imewakosa watoto wenye maarifa.

Aidha, amesema kuwa wanafunzi hao wanaotoka katika familia zenye uhitaji husoma na kupata elimu yao katika hali ya majonzi hivyo jamii kwa pamoja inapaswa kuwaunga mkono wote wanaojitokeza katika kuunga mkono mpango huo wa kutoa elimu bure kwa kujitolea vifaa vya kujifunzia.

Naye Kaimu Afisa wa Elimu wilaya ya Chamwino Abraham Msigwa amesisitiza suala la kujitolea kwa ajili ya maendeleo ya elimu katika kuwawezesha wanafunzi namna ya kujifunza huku baadhi ya wanafunzi wakikiri kuwa vifaa vya kujifunzia ni changamoto miongoni mwao.

WAZIRI JAFO ATOA RAI KWA JAMII NCHINI KUUNGA MKONO MPANGO WA SERIKALI WA ELIMU BURE WAZIRI JAFO ATOA RAI KWA  JAMII NCHINI KUUNGA MKONO MPANGO WA SERIKALI WA ELIMU BURE Reviewed by safina radio on February 08, 2018 Rating: 5

No comments