Rais wa Urusi, Vladimir Putin amezungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron pamoja na Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kuhusu machafuko ya nchini Syria.
MOSCOW.
Rais wa Urusi,
Vladimir Putin amezungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel
Macron pamoja na Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kuhusu machafuko ya nchini
Syria.
![]() |
Rais wa Urusi, Vladimir Putin amezungumza kwa njia ya simu na baadhi ya viongozi wa Umoja wa Ulaya. |
Kwa mujibu wa Ikulu ya rais wa Urusi, katika
mazungumzo yao, viongozi hao wameangazia umuhimu wa jitihada za pamoja
kuutekeleza mkataba wa kusitisha mashambulizi kwa siku 30 uliopitishwa na Umoja
wa Mataifa.
Msemaji wa serikali
ya Ujerumani amesema, Merkel na Macron wamemhimiza Putin kuongeza shinikizo
zaidi kwa utawala wa Syria kusitisha mashambulizi ya angani na mashambulizi
mengine Ghouta Mashariki.
Taarifa imesema
Merkel, Macron na Putin wameukubali uamuzi wa Umoja wa Mataifa hasa kuruhusu
misaada kufikishwa na kuondolewa kwa watu katika eneo la vita.
Hata hivyo Wamesisitiza
kuwa kusitishwa kwa mashambulizi kutawezesha kuanzishwa kwa juhudi za kutafuta
suluhisho la kisiasa.
Rais wa Urusi, Vladimir Putin amezungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron pamoja na Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kuhusu machafuko ya nchini Syria.
Reviewed by safina radio
on
February 26, 2018
Rating:

No comments