KISIWA CHA TONGA KIMEPIGWA NA KIMBUNGA NA KUSABABISHA MAFURIKO MAKUBWA.
TAREHE 13-02-2018
Kimbunga Gita kinachoorodheshwa kuwa
cha kiwango cha nne kimepiga kisiwa cha Tonga ambacho ni miongoni mwa visiwa
vya bahari ya Pasifiki mapema hii leo na kusababisha mafuriko makubwa pamoja na
kuharibu mifumo ya umeme.
Maafisa wa nchi hiyo wanakielezea
kimbunga Gita kuwa ni kikali zaidi kuwahi kupiga mji mkuu wa kisiwa hicho,
Nuku'alofa.
Kimbunga hicho kimekipiga kisiwa cha
Tonga na kusababisha uharibifu mkubwa kutokana na upepo mkali wa kiasi cha
mwendo wa kilomita 233 kwa saa, na kuharibu takribani asilimia 40 ya makazi
katika mji huo mkuu.
Hakukua na taarifa yoyote ya vifo
vilivyosababishwa na dhoruba hiyo, lakini wengi wamejeruhiwa, baadhi yao
vibaya.
Visiwa vingine vilivyopo bahari ya
Pasifiki pia vitapigwa na kimbunga Gita wakati kikielekea Fiji, Vanatu na New
Caledonia katika siku chache zijazo.
KISIWA CHA TONGA KIMEPIGWA NA KIMBUNGA NA KUSABABISHA MAFURIKO MAKUBWA.
Reviewed by safina radio
on
February 13, 2018
Rating:

No comments