MAGAIDI 23 WA AL-SHABAB WAUAWA NA JESHI LA KENYA KWA KUSHIRIKIANA NA SOMALIA LIMEUA


MOGADISHU.
Jeshi la Kenya likishirikiana na Jeshi la Somalia, limewauwa magaidi 23 wa Al Shabab katika mji wa Fahfahdun Kusini Magharibi mwa mkoa wa Gedo nchini Somalia.
Jeshi la Kenya likishirikiana na Jeshi la Somalia, limewauwa magaidi 23 wa Al Shabab katika mji wa Fahfahdun







Ripoti zinasema magaidi hao waliuawa wakati wanajeshi wa Kenya chini ya mwavuli wa AMISOM walipokuwa wanafanya oparesheni ya kulenga ngome mpya za magaidi hao.
Makabiliano makali yalishuhudiwa kwa muda wa saa nne kati ya wanajeshi wa AMISOM na magaidi hao waliokuwa wamejihami kwa silaha hatari.
Majeshi ya Kenya KDF na yale ya Somalia SDF, yanasema mbali na mauaji hayo, walifanikiwa kuwapokonya magaidi hao silaha na kuteketeza moto magari kadhaa pamoja na kambi yao.
Kenya ilituma jeshi lake nchini Somalia mwaka 2011, baada ya Al Shabab kuwateka nyara wafanyikazi wawili wa Kihispania waliokuwa wanalifanyia kazi Shirikila la Madaktari wasiokuwa na mipaka MSF, katika kambi ya Daadab nchini Kenya
MAGAIDI 23 WA AL-SHABAB WAUAWA NA JESHI LA KENYA KWA KUSHIRIKIANA NA SOMALIA LIMEUA MAGAIDI 23 WA AL-SHABAB WAUAWA NA JESHI LA KENYA KWA KUSHIRIKIANA NA SOMALIA LIMEUA Reviewed by safina radio on February 28, 2018 Rating: 5

No comments