MANDA AAGIZA KUKAMATWA KWA WAZAZI WANAODAIWA KUWAFUNDISHA WATOTO KUJAZA MAJIBU YA UONGO.
MTWARA.
Taarifa ya Habari 01:00 mchana, 15 February, 2018.
![]() |
Mkuu wa Wilaya Evod Manda. |
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Manda
ameagiza kukamatwa kwa wazazi wanaodaiwa kuwafundisha watoto kujaza majibu ya uongo
katika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kwa kuogopa gharama za kuwapeleka wanafunzi
shule za sekondari.
Manda ametoa agizo hilo katika kikao
cha wadau wa elimu wa halmashauri ya Nanyamba kufuatia shule zaidi ya tano
kubainika kuwa baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa shule hizo wamewafundisha watoto
wao kujaza majibu ya uongo kwenye mitihani yao ya kumaliza darasa la saba ili
wafeli katika mitihani yao.
Aidha, amewataka walimu na wazazi
kushirikiana ili kuweza kubaini na kuwapata wazazi ambao wanawashawishi watoto
wao kuandika majibu ya uongo katika mitihani yao ambapo pia amesema sheria ya elimu
inakataza na inatoa adhabu kwa mtu yeyote anayemzuia mtoto kwenda shule.
Kwa upande wao maafisa elimu wa msingi
na sekondari katika halmashauri ya Nanyamba wamesema kuwa wamejipanga
kuhakikisha wanafuatilia shule na walimu ili wanafunzi wafanye vizuri katika masomo yao,
hii ikiwa ni kutokana na halmashauri
hiyo kuwa nyuma kielimu.
Hata hivyo wadau wa elimu walioshiriki
katika kikao hicho wametoa maoni yao katika suala hilo huku wakiitaka serikali kuingilia
kati suala la elimu na kuboresha miundombinu ya elimu katika Halmashauri hiyo.
MANDA AAGIZA KUKAMATWA KWA WAZAZI WANAODAIWA KUWAFUNDISHA WATOTO KUJAZA MAJIBU YA UONGO.
Reviewed by safina radio
on
February 15, 2018
Rating:

No comments