MKUCHIKA, MFUKO WA RAIS KUJITEGEMEA ILI KUTOA HUDUMA NCHINI KOTE.


DAR-ES-SALAAM.
Taarifa ya Habari saa 08:00 usiku, 13 February, 2018.
Kaptein George Mkuchika, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Ututumishi wa Umma na Utawala Bora.
Waziri wa nchi ofisi ya rais Menejimenti ya Ututumishi wa Umma na Utawala Bora Kaptein George Mkuchika amesema kuwa serikali itatekeleza azma ya bunge ya kutaka mfuko wa rais wa kujitegemea kutoa huduma nchini kote.
Akizungumza na Watumishi wa Mfuko huo jijini Dar es salaam Mh. Mkuchika amesema kuwa baadhi ya watu wanakosa fursa ya maendeleo kwa kuwa huduma za mfuko huo hazifiki nchi nzima.
Mkurugenzi wa Mfuko huo Haigati Kitala amesema kupitia mfuko huo wananchi wengi wamepata hari na mwamko ya kuanzisha miradi ya maendeleo.
Hata hivyo, kwa sasa mfuko wa rais wa kuwezesha wananchi kiuchumi unafanya shughuli zake kwa mikoa ya Dar es salaam, Iringa, na Morogoro.

MKUCHIKA, MFUKO WA RAIS KUJITEGEMEA ILI KUTOA HUDUMA NCHINI KOTE. MKUCHIKA, MFUKO WA RAIS KUJITEGEMEA ILI KUTOA HUDUMA NCHINI KOTE. Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments