RAMAPHOSA ASEMA KUWA HATIMA YA RAIS JACOB ZUMA ITAJULIKANAQ SIKU CHACHE ZIJAZO.


TAREHE 08-02-2018

Mwenyekiti Taifa wa chama tawala cha ANC cha Afrika Kusini amesema kuwa, hatima ya Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo itajulikana siku chache zijazo.
Mwenyekiti huyo ambaye ni Bw Cyril Ramaphosa amesema kuwa, tayari ameanza mazungumzo na Rais Jacob Zuma kuhusiana na suala la kukabidhi madaraka na masuala mengineyo.
Ameongeza kuwa, matokeo ya mazungumzo yao yatajulikana siku chache zijazo na wakati huo ndipo itajulikana hatima ya Rais Jacob Zuma.
Ramaphosa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Afrika Kusini amesema, mazungumzo yake na Jacob Zuma yalikuwa mazuri na yamechunguza njia bora na za haraka za kutatua matatizo ya nchi hiyo.
Rais Jacob Zuma amezidi kuwa chini ya mashinikizo ya chama tawala cha ANC tangu Cyril Ramaphosa alipochaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho.
Iwapo Jacob Zuma atajiuzulu, Cyril Ramaphosa ambaye ni makamu wake atachukua uongozi wa Afrika Kusini hadi utakapoitishwa uchaguzi mwingine wa rais mwaka 2019.

RAMAPHOSA ASEMA KUWA HATIMA YA RAIS JACOB ZUMA ITAJULIKANAQ SIKU CHACHE ZIJAZO. RAMAPHOSA ASEMA KUWA HATIMA YA RAIS JACOB ZUMA ITAJULIKANAQ SIKU CHACHE ZIJAZO. Reviewed by safina radio on February 08, 2018 Rating: 5

No comments