NAIBU WAZIRI WA HABARI, JULIANA SHONZA AWATAKA WAANDISHI KUZINGATIA MISINGI KATIKA UTOAJI TAARIFA NA UCHAPISHAJI HABARI.


DODOMA.
Taarifa ya Habari saa 08:00 usiku, 13 February, 2018.
Mh Juliana Shonza Naibu waziri wa habari utamaduni sanaa michezo.
Naibu waziri wa habari utamaduni sanaa michezo Mh Juliana Shonza amewataka waandishi wa habari hapa nchini kuacha kujiingiza katika masuala ya siasa na badala yake wazingate msingi katika utoaji wa taarifa na upashanaji habari kwa mujibu wa sheria ya huduma ya vyombo vya habari.
Mh Shonza ameyasema hayo mjini Dodoma alipokutana na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni siku ya maadhimisho ya redio duniani ambapo kitaifa yamefanyika huko mkoani Dodoma.
Naibu waziri huyo ameeleza kuwa vyombo vya habari ni mhimili mkuu unaotegemewa kufikisha elimu katika jamii hivyo havipaswi kujiingiza katika upande wowote wa siasa.
Aidha, amesema kuwa baadhi ya waandishi wa habari kutokuzingatia lugha fasaha ya Kiswahili na kuchanganya baadhi ya maneno ya kigeni imekuwa ni tatizo linalosababisha jamii hapa nchini kutokupata habari zinazoweza kuwasaidia kujiendeleza kimaendeleo.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Bilinith Mahenge kwa kutambua umuhimu wa vyombo vya habari amesisitiza waandishi kutumia kalamu na uweledi wao kuitangaza Dodoma na fursa zinazopatikana hapa nchini.

NAIBU WAZIRI WA HABARI, JULIANA SHONZA AWATAKA WAANDISHI KUZINGATIA MISINGI KATIKA UTOAJI TAARIFA NA UCHAPISHAJI HABARI. NAIBU WAZIRI WA HABARI, JULIANA SHONZA AWATAKA WAANDISHI KUZINGATIA MISINGI KATIKA UTOAJI TAARIFA NA UCHAPISHAJI HABARI. Reviewed by safina radio on February 13, 2018 Rating: 5

No comments