RAIS WA ZAMANI WA PERU ALBERTO FUJIMORI KUSHTAKIWA KWA MAUAJI

TAREHE 20-02-2018



Rais wa zamani wa Peru ambaye alipewa msamaha hivi karibuni Alberto Fujimori, atashitakiwa kwa mauaji ya mwaka 1992 ya wakulima sita, mahakama imetoa uamuzi huo siku ya Jumatatu.

Uamuzi huo unakuja wiki chache baada ya kiongozi huyo wa zamani, kupewa msamaha uliojaa utata na kuachiwa kutoka kifungo cha miaka 25 jela kwa makosa ya ukiukaji wa haki za binadamu alioufanya kati ya mwaka 1999 na 2000 wakati akiwa madarakani.

Lakini mahakama siku ya jumatatu ilitupilia mbali utetezi wake kwamba msamaha huo pia unajumuisha kesi ya Pativilca, jina la wilaya ambako mauaji hayo yalitokea.

Wakosoaji wanasema rais wa sasa Pedro Pablo Kuczynski ambaye alikuwa anakabiliwa na kura ya kutokuwa na imani naye, alitoa msamaha kama malipo kwa mtoto wa Fujimori ambaye ni mbunge na wenzake kutopiga kura ya kumuondoa madarakani.

RAIS WA ZAMANI WA PERU ALBERTO FUJIMORI KUSHTAKIWA KWA MAUAJI RAIS WA ZAMANI WA PERU ALBERTO FUJIMORI KUSHTAKIWA KWA MAUAJI Reviewed by safina radio on February 20, 2018 Rating: 5

No comments