WATU 20 WAMEFARIKI NCHINI INDIA
Katika oparesheni dhidi ya wanaopigania kujitenga zilizoanza
Jumamosi usiku, wanamgambo wasiopungua 13 wameuawa. 
Aidha Jeshi la India limesema wanajeshi wake watatu wameuawa
huku raia wanne nao wakipoteza maisha katika mapigano hayo.
Maandamano makubwa yameripotiwa Kashmir hasa katika mji wa
Srinigar ambapo makundi yanaopigania kujitenga yameitisha mgomo leo Jumatatu
Kashmir ni jimbo lenye Waislamu wengi India na limekuwa
likikumbwa na mzozo tokea India ipate uhuru kutoka Uingereza mwaka 1947.
Eneo lingine la Kashmir liko Pakistan ambayo pia ilikuwa koloni
la Uingereza. Wakazi wa Kashmir wanataka kujitenga na India na kutangza
dola lao huru au kujiunga na Pakistan.
WATU 20 WAMEFARIKI NCHINI INDIA
Reviewed by safina radio
on
April 02, 2018
Rating:
No comments