WAZIRI WA AFYA UMMY MWALIMU AMETOA MAAGIZO KWA WAGANGA WAKUU WA WILAYA NA MIKOA NCHINI.


Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewaagiza waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya Nchini kuhakikisha kuwa wasimasamizi wote wa vituo vya afya na zahanati wanaandika orodha ya dawa na vipimo vinavyopaswa kutolewa bure na kubandika katika ubao wa matangazo.

Image result for PICHA YA UMMY MWALIMU
WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU.
Waziri Ummy ametoa maagizo hayo Mkoani Kigoma wakati wa kugawa vyandarua kwa wamama Wajawazito katika Kituo cha Afya cha Mwandiga.=
Mh. Ummy amewataka wasimazi wa vituo vya afya vya serikali waandike katika mbao za matangazo kuwa kipimo cha malaria, dawa mseto na sindano ya malaria kali ni bure na hakuna malipo yoyote mgonjwa anatakiwa kulipa.
Hata Hivyo, Zoezi hilo la ugawaji wa vyandarua vimeenda sambamba na maonyesho ya utolewaji wa huduma za matibabu ugonjwa wa malaria kwa wananchi.   

WAZIRI WA AFYA UMMY MWALIMU AMETOA MAAGIZO KWA WAGANGA WAKUU WA WILAYA NA MIKOA NCHINI. WAZIRI WA AFYA UMMY MWALIMU AMETOA MAAGIZO KWA WAGANGA WAKUU WA WILAYA NA MIKOA NCHINI. Reviewed by safina radio on April 25, 2018 Rating: 5

No comments