ASKARI NA MAAFISA WA JWTZ WANAOSHIRIKI ZOEZI LA ULINZI NCHINI SUDANI WATUNUKIWA NISHANI NA UMOJA WA MATAIFA.


Askari na Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania JWTZ wanaoshiriki ulinzi wa amanai nchini Sudani wametunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa na kutakiwa kulinda sifa na heshima nzuri la jeshi hilo kitaifa na kimataifa.

Image result for PICHA YA LUTEN JENERALI LEONARD NGONDI MKUU WA KIKOSI CHA ULINZI NCHINI SUDANI


Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Amani katika Jimbo la Dafur Luten Jeneral Leonard Ngondi amesema kuwa Nisahini hizo ni ishara ya mafanikio ya kazi nzuri iliyofanywa na majeshi kutoka Tanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa Operesheni wa kundi kazi katika safu za milima ya Jabar Mara, Lameki Kawite amesema kuwa kilichooneshwa na wanajeshi hao wakati wa utumishi na maonesho wakati wa sherehe ni ishara tosha kuwa jeshi la Tanzania liko imara.

Hata hivyo katika kipindi chote cha uwajibikaji JWTZ imefanikiwa kufika katika maeneo ambayo hayakuwahi kufikiwa licha ya chanagamoto za miundombinu ambapo kwa sasa imejumuishwa katika kikosi kazi maalumu kitakachofanya kazi katika safu za milima ya Jabar Mara ambayo hukaliwa na waasi.

ASKARI NA MAAFISA WA JWTZ WANAOSHIRIKI ZOEZI LA ULINZI NCHINI SUDANI WATUNUKIWA NISHANI NA UMOJA WA MATAIFA. ASKARI NA MAAFISA WA JWTZ WANAOSHIRIKI ZOEZI LA ULINZI NCHINI SUDANI WATUNUKIWA NISHANI NA UMOJA WA MATAIFA. Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.