WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA BIDHAA ZA SOKO LA NDANI.


Naibu waziri wa viwanda biashara na uwekezaji Mh Stella Manyanya amewataka watanzainia kutumia bidhaa za soko la ndani ikiwemo zao la mbaazi kuliko kutegemea watu wa njee kutumia bidhaa hizo.

Image result for PICHA YA STELLA MANYANYA
MH. MANYANYA
Mh Manyanya ametoa ushauri huo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Mtama Mh Nape Nnawiye aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kutafuta soko la zao la mbaazi ambalo kwa kiasi kikubwa limeshuka bei kutokana na kukosekana kwa soko la uhakika.


Amesema kuwa hapo awali serikali ilikuwa inategemea soko la mbaazi kutoka nchini India lakini baada ya India kujitosheleza na bidhaa hiyo zao la mbaazi lilikosa soko hali iliyosababisha kushuka bei kutoka shilingi elfu mbili kwa kilo hadi shilingi mia moja na hamsini msimu uliopita.

Ameongeza kuwa wakati huu ambapo serikali inaendelea kutafuta soko wananchi wanatakiwa kununua na kutumia bidhaa hiyo kwani kwa sasa bidhaa hiyo imeanza kupanda,ambapo katika masoko mbalimbali ya mkoa wa Dodoma mbaazi inauzwa Zaidi ya shilingi elfu moja kwa kilo huku katika Supermarket za mkoa wa Dar-es-Salaam ikiuzwa kwa Zaidi ya shilingi elfu mbili.

Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti ya ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 iliyowasilishwa hapo jana na waziri wa ofisi hiyo Mh January Mkamba.



WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA BIDHAA ZA SOKO LA NDANI. WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA BIDHAA ZA SOKO LA NDANI. Reviewed by safina radio on April 17, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.