BUNGE LA BURUNDI LAPITISHA SHERIA POLISI KUAGUA NYUMBA ZA RAIA BILA KIBALI MAALUMU.
Bunge
nchini Burundi limepitisha mswada wa sheria uliyowasilishwa na Waziri wa
Sheria, kuruhusu polisi kufanya ukaguzi katika makazi ya watu bila kibali
maalum.
Waziri wa Sheria Aimé Laurentine
Kanyana aliutetea mswada huo kwa kile alichokitaja kuwa Burundi inakabiliwa na
visa vya mauaji ya kikatili,ugaidi, baishara ya binadamu na kumiliki silaha
kinyume cha sheria, utumiaji wa dawa za kulevya na hata ubakaji.
Vyanzo vya habari vinaeleza kuwa
mswada huo umepitishwa kwa kura 97 huku ukipingwa kwa kura 22 za wabunge wa
upinzani, hatua ambayo imekosolewa
vikali na wapinzani na watetezi wa haki za binadamu nchini humo.
Vyama vya upinzani nchini humo,
vimehofia utaratibu huo, ambapo mkuu wa chama cha upinzani, UPRONA, Abel
Gashatsi ameeleza, kuwa Nchi ya Burundi imetoka katika vita, hivyo ni lazima
watu waogope.
Kwa upande wa chama kikongwe cha
upinzani, FRODEBU wanasema muswada huo unakiuka katiba na kupendekeza baraza la
Seneti kuurejesha na kuupinga.
BUNGE LA BURUNDI LAPITISHA SHERIA POLISI KUAGUA NYUMBA ZA RAIA BILA KIBALI MAALUMU.
Reviewed by safina radio
on
April 20, 2018
Rating:
No comments