URUSI KUPENDEKEZA WACHUNGUZI WA KIMATAIFA
SERGEI LAVROV |
Hatua hiyo imekuja baada ya kitisho cha Rais
wa Marekani Donald Trump kuichukulia hatua ya haraka za kijeshi dhidi ya serikali
ya Syria baada ya shambulio hilo la kemikali kutokea.
Rais wa Syria Bashar
al-Assad pamoja na Urusi ambayo ni mshirika wake wa karibu, wamesema hakuna
ushahidi unaoonesha kuwa kumefanyika
shambulio la kemikali na kwamba madai hayo hayana msingi.
Aidha, Waziri wa
Mambo ya Nje wa Urusi Sagey Lavrov amesema kuwa mara kadhaa wamekwisha eleza
kuwa Wawakilishi wa Shirika la Msalaba Mwekundu la Syria na wawakilishi wa
Kirusi ambao wanasimamia usalama wa redilojia wametembelea eneo linaloshukiwa
kutokea tukio hilo huko Douma na hawajaona tatizo lolote la kemikali.
Hata hivyo Takriban
watu 60 wameuawa na wengine zaidi ya elfu moja wamejeruhiwa katika maeneo
kadhaa katika shambulio linalodaiwa kutokea katika mji wa Douma, ambao kwa
wakati huo ulikuwa bado unadhibitiwa na vikosi vya waasi.
URUSI KUPENDEKEZA WACHUNGUZI WA KIMATAIFA
Reviewed by safina radio
on
April 11, 2018
Rating:
No comments