HOSPITALI YA MANISPAA YA IRINGA FRELIMO YAKABILIWA NA UKOSEFU WA VIFAA.


 Ukosefu wa baadhi ya miundombinu na vifaa tiba katika hospitali ya Manispaa ya Iringa ya FRELIMO umesababisha kushindwa kutoa huduma kwa ufanisi kwa wagonjwa wanaofika hospitalini hapo.

Image result for PICHA YA HOSPITALI YA MANISPAA YA IRINGA FRELIMO
MAJENGO YA HOSPITALI YA MANISPAA YA IRINGA FRELIMO
Aidha Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dk. Pilila Zambi amesema kuwa hospitali hiyo kwa sasa inawahudumia wananchi zaidi ya laki mbili na hivyo kuzidiwa uwezo kutokana na kukosa baadhi ya majengo muhimu ikiwemo jengo la kuhifadhia maiti.

Kufuatia hali hiyo Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Bw Omary Mkangama amesema kuwa Halmashauri ya Manispaa hiyo imetenga bajeti ya kiasi cha fedha milioni 100 ili kutatua baadhi ya changamoto kwa awamu.

Aidha, Halmashauri hiyo ya Manispaa ya Iringa inaendelea kuwatafuta wadau mbali mbali ili kuhakikisha kuwa changamoto zinazoikumba hospitali hiyo zinatatuliwa.

HOSPITALI YA MANISPAA YA IRINGA FRELIMO YAKABILIWA NA UKOSEFU WA VIFAA. HOSPITALI YA MANISPAA YA IRINGA FRELIMO YAKABILIWA NA UKOSEFU WA VIFAA. Reviewed by safina radio on April 11, 2018 Rating: 5

No comments