SERIKALI KUENDELEA KUPUNGUZA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZINAZOZIKABILI SHULE ZA SEKONDARI NCHINI.



Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI)  Mh Joseph Kakunda amesema kuwa serikali itaendelea kupunguza changamoto mbalimbali zinazokabili shule za sekondari hapa nchini ikiwemo upungufu wa waalimu wa sayansi.

Image result for PICHA YA JOSEPH KAKUNDA NAIBU WAZIRI TAMISEMI
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI MH.  KAKUNDA.

Mh Kakunda ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mh Hamidu Mobali aliyetaka kujua ni lini serikali itamaliza tatizo la upungufu wa waalimu wa shule za sekondari hapa nchini.

Amesema kuwa mpango uliopo kwa sasa ni serikali kuwaajiri walimu wa sayansi wapatao mia sita kufikia Juni 30 mwaka huu lengo likiwa ni kuondoa kabisa tatizo la waalimu wa sayansi na hisabati katika shule za sekondari ifikapo mwaka wa 2020.

Katika hatua nyingine Mh Kakunda amesema kuwa serikali haijakataza michango ya wananchi ya kusaidia kujenga miundombinu ya shule ikiwemo maabara ila serikali ilichokataza ni kumpa mwanafunzi adhabu ya kukosa masomo kutokana na mzazi wake kutotoa michango.

Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti za wizara mbalimbali kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.

SERIKALI KUENDELEA KUPUNGUZA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZINAZOZIKABILI SHULE ZA SEKONDARI NCHINI. SERIKALI KUENDELEA KUPUNGUZA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZINAZOZIKABILI SHULE ZA SEKONDARI NCHINI. Reviewed by safina radio on April 16, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.