WABUNGE WATAKIWA KUCHUKUA HATUA STAHIKI KUDHIBITI UNYANYASAJI WA KIJINSIA.


Wabunge wametakiwa kuchukua hatua stahiki kudhibiti vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinavyofanywa dhidi ya wanawake na watoto wenye walemavu.

Image result for PICHA YA BUNGE LA TANZANIA


Ushauri huo umetolewa kwa wabunge baada ya utafiti uliofanywa na shirika la Action On Disabillity and Development kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye ulemavu kubaini kuwepo kwa baadhi ya udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto wenye ulemavu.

Utafiti huo umewekwa bayana kwa wabunge ambapo inadaiwa kuwa baadhi ya ndugu na jamaa wamekuwa wakishirikiana kufanya vitendo vya udhalilishaji wanawake na watoto wenye ulemavu hususani wenye ulemavu wa kusikia na akili.

Baadhi ya wabunge wamedai kuwa utaratibu wa elimu jumuishi ni moja njia muhimu itakayoweza kupunguza matatizo ya walemavu ikiwa shule za msingi na sekondari zitapatiwa vifaa, wataalamu na miundombinu ya kuwezesha watu wenye ulemavu kupata elimu pamoja na wanafunzi wengine wasio na ulemavu.




WABUNGE WATAKIWA KUCHUKUA HATUA STAHIKI KUDHIBITI UNYANYASAJI WA KIJINSIA. WABUNGE WATAKIWA KUCHUKUA HATUA STAHIKI KUDHIBITI UNYANYASAJI WA KIJINSIA. Reviewed by safina radio on April 23, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.