ZANA HARAMU ZA UVUVI ZAKAMATWA MKOANI MWANZA


Operesheni Sangara awamu ya pili imefanikiwa kukamata zana haramu za uvuvi pamoja na injini tano za boti zinazosadikika kuwa ni za wizi zikiwa zimefukiwa ardhini kwenye eneo la nyumba ya mfanyabiashara mmoja wa samaki mkoani Mwanza.

Image result for PICHA YA ZANA HARAMU ZA UVUVI


Afisa Uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Kanerd Katunusi amesema kuwa nyavu hizo zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni hamsini ni miongoni mwa zana za Uvuvi ambazo zilipigwa marufuku kutokana na madhara yake kwa viumbe vya ziwani.

Aidha Afisa Uvuvi huyo wa Halmashauri ya jiji la Mwanza amesema kuwa zana hizo zimepatikana baada ya maafisa wa kikosi maalumu cha kupambana na uvuvi haramu katika ziwa Victoria Wilayani Nyamagana kufukua shimo moja kwenye ua wa nyumba ya mfanyabiashara huyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Mwananchi Elifance Masinde amesema kuwa zana hizo haramu zimekutwa zimefukiwa kwenye eneo la nyumba Kondo na eneo la Mtaa wake wa  Mwananchi jijini Mwanza.

Katika Operesheni hiyo kumebainika kuwa injini tano za boti zilizokutwa kwenye shimo hilo zina thamani ya zaidi shilingi milioni ishirini  zinazosadikiwa kuwa ni za wizi huku watu waliokutwa katika makazi ya mfanyabiashara huyo wakishikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi.




ZANA HARAMU ZA UVUVI ZAKAMATWA MKOANI MWANZA ZANA HARAMU ZA UVUVI ZAKAMATWA MKOANI MWANZA Reviewed by safina radio on April 24, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.