ANGELA MERKEL KUKUTANA NA TRUMP


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel atakutana leo na Rais wa Marekani Donald Trump katika Ikulu ya White House, akikabiliwa na kibarua kigumu cha kuukoa muafaka wa nyuklia wa Iran, kuepusha vita vya kibiashara na kuyafanya mahusiano yake na rais huyo wa Marekani kuanza tena kufanya kazi.
Image result for PICHA YA TRUMP NA ANGELA MERKEL 

Ziara ya kiongozi huyo wa Ujerumani tayari imegubikwa na mazungumzo yaliyoonekana kuwa ya undugu kati ya Donald Trump na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron wiki hii.

Saa chache tu kabla ya Kansela Merkel kutua jana usiku nchini Marekani, ikiwa ni miezi 15 baada ya Trump kuapishwa kuwa rais, Bunge la Marekani hatimaye lilifanikiwa kumuidhinisha balozi wa nchi hiyo nchini Ujerumani.

Hata hivyo  Muda mfupi baada ya uteuzi wake, Richard Grenell  anayejulikana kwa msimamo wake wa kihafidhina na mtetezi mkubwa wa sera za Trump za ``Marekani Kwanza” alithibitishwa kuchukua wadhifa huo.

ANGELA MERKEL KUKUTANA NA TRUMP ANGELA MERKEL KUKUTANA NA TRUMP Reviewed by safina radio on April 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.