WAAJIRI NCHINI WAMETAKIWA KUWASILISHA MAJINA YA WAFANYAKAZI BODI YA MIKOPO


Waajiri kote nchini ambao hawajawasilisha majina ya wafanyakazi kwenye  bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa ajili ya uhakiki wametakiwa kufanya hivyo kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Image result for PICHA YA BW. FIDELIS JOSEPH MKURUGENZI MSAIDIZI UREJESHAJI MIKOPO
BW. PHIDELIS JOSEPH

Akizungumza jijini Mwanza alipotembelea hospitali ya Uhuru Mkurugenzi Msaidizi Urejeshaji Mikopo wa Bodi hiyo Bw. Fidelis Joseph amesema kuwa baadhi ya waajiri hawajawasilisha majina ya wafanyakazi wao kwenye bodi hiyo.

Aidha, amebainisha kuwa tatizo la watendaji kutokutoa ushirikiano kwa watumishi wa Bodi huku akisema kuwa sheria ya bodi hiyo inaeleza kuwa endapo mtu yeyote atawazuia watendaji hao wa bodi anaweza kukamatwa mara moja na kupelekwa katika maeneo ya kisheria.

Wakiwa jijni humo maafisa wa bodi hiyo wametembelea hospitali ya uhuru na shule za Allience na kubaini kuwa zaidi ya wafanyakazi mia moja,majina yao hayajawasilishwa kwenye bodi ya mikopo kwa ajili ya kuhakikiwa.

WAAJIRI NCHINI WAMETAKIWA KUWASILISHA MAJINA YA WAFANYAKAZI BODI YA MIKOPO WAAJIRI NCHINI WAMETAKIWA KUWASILISHA MAJINA YA WAFANYAKAZI BODI YA MIKOPO Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.