VIONGOZI NA RAIA WA KENYA WATOA WITO KWA TUME YA UCHAGUZI KUVUNJWA.
Viongozi
na raia wa Kenya wametoa wito wa kuvunja tume ya uchaguzi baada ya makamishna
watatu kujiuzulu kutokana na migongano ya siasa isiyoisha.

Migongano
hiyo imeanza mwaka jana kwenye vipindi viwili vya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo,ambapo
makamishna watatu wa tume ya uchaguzi wamejiuzulu juzi nyadhifa zao za uongozi
ndani ya tume hiyo.
Aidha,
duru za habari zinaeleza kuwa makamishna hao waliojiuzulu nyadhifa zao za
uongozi ni pamoja na Consalata Maina, Paul Kurgat na Margaret Mwachanya .
Habari
zinaeleza kuwa kiwango cha imani ya wananchi dhidi ya tume hiyo kimeshuka
zaidi, na inaonekeana kuwa kuvunjwa kwa tume hiyo ndio njia pekee ya kutatua suala
hilo.
Hata
hivyo kwa mujibu wa sheria, makamishna watano kati ya saba wa tume hiyo
wanaweza kufanya maamuzi, lakini kwa vile sasa kuna ukosefu wa makamishna
watatu, tume hiyo haiwezi kufanya kazi ipasavyo.
VIONGOZI NA RAIA WA KENYA WATOA WITO KWA TUME YA UCHAGUZI KUVUNJWA.
Reviewed by safina radio
on
April 18, 2018
Rating:

No comments