MAPADRI WAWILI WAUAWA NA WAUMINI 16 NCHINI DRC.
Mapadri
wawili wa kanisa Katoliki na waumini 16 wa kanisa hilo wameuawa katika
shambulizi lililotokea katika kijiji cha Mbalom katika jimbo la Benue, nchini
Nigeria siku ya jana.
Shambulizi
hilo lililotokea katikati mwa nchi ambako kumeendelea kushuhudiwa mapigano ya
kikabila yanayohusisha wafugaji waliokua
wamebeba silaha,ambapo washambuliaji hao waliingia katika kanisa wakati wa
sherehe ya mazishi katika kijiji cha Mbalom, katika jimbo la Benue, nchini
Nigeria.
Mapadri
wawili na waumini 16 wa kanisa Katoliki, wote waliuawa kwa kupigwa risasi, kwa
mujibu wa mashahidi walionukuliwa na shirika la habari la AFP ambao pia
wamesema watu wengi walijeruhiwa.
Dayosisi
ya Makurdi, mji mkuu wa Jimbo la Benue, imelaani vurugu ambazo zilikumba
mojawapo ya makanisa yake huku Rais
Muhammadu Buhari wa nchi hiyo akiahidi kuwaadhibu wale wote waliohusika na
katika tukio hilo kwa mujibu wa sheria.
MAPADRI WAWILI WAUAWA NA WAUMINI 16 NCHINI DRC.
Reviewed by safina radio
on
April 25, 2018
Rating:
No comments