HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAFUNDISHO NA MAOMBI KWA AJILI YA KUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU NDANI YA MTU.


Imebainishwa kuwa baadhi ya watu wameshinda kutambua kusudi la Mungu lililoko ndani yao jambo ambalo linawafanya waendelee kuishi maisha duni kutokana na kushindwa kumudu kazi zao kama vile biashara,Afya,kilimo,ufugaji na huduma kwa ujumla.

Image result for radio safina

Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa saba mchana  imekuandalia mafundisho na maombi maalum kuhusu namna ya kutambua kusudi lililowekwa na Mungu ndani ya mtu.

Kutokana na watu wengi kushindwa kutambua kusudi la Mungu waliloliwekewa ndani yao wamejikuta wakikumbana na matatizo mbalimbali ikiwemo magonjwa,kuporomoka kwa uchumi,kukosa kazi,kutokuoa au kuolewa huku wengine wakikosa watoto na mara nyingine mimba kuharibika.

Sambamba na hayo kesho kutafanyika maombi maalum ya kufufua vipawa na karama kama vile huduma,biashara kilimo ufugaji, vyote ambavyo vilikuwa vimeshikiliwa na adui kwa muda mrefu na kusababisha Baraka kutokufikia watu kwa wakati.

 Hali kadhalika kesho watu wenye mahitaji mbalimbali wataombewa ili kufunguliwa dhidi magonjwa,madeni na nguvu za giza.

HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAFUNDISHO NA MAOMBI KWA AJILI YA KUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU NDANI YA MTU. HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAFUNDISHO NA MAOMBI KWA AJILI YA KUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU NDANI YA MTU. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.