WATU 63 WAPOTEZA MAISHA MJINI KABUL.


Watu 63 wamepoteza maisha jijini Kabul nchini Afghanistan baada ya kutokea kwa mashambulizi ya bomu katika maeneo mbalimbali ya kujiandikisha wapiga kura.
Mmoja wa mtoto aliyeshambuliwa na Bomu Afghanstan
MAJERUHI WAKIPATIWA MATIBABU
Taarifa kutoka mamlaka mjini Kabul zinasema kuwa wanawake 21 na watoto watano ni miongoni mwa waliouawa na watu 119 wamejeruhiwa katika mashambulizi hayo.
Mlipuko huo pamoja na kusababisha vifo  umeharibu magari ,ambapo hadi sasa kumekuwa na mashambulio manne tangu kuanza uandikishaji huo wiki iliyopita.
Kundi la Islamic State limesema ndilo lililohusika na shambulizi hilo lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita.
Hata hivyo Kazi ya uandikishaji wapiga kura nchini humo imeanza mwezi uliopita ikiwa ni maandalizi kwaajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.








WATU 63 WAPOTEZA MAISHA MJINI KABUL. WATU 63 WAPOTEZA MAISHA MJINI KABUL. Reviewed by safina radio on April 23, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.