UFARANSA KULIPIZA KISASI
Ufaransa imesema italipiza
kisasi dhidi ya utawala wa Syria wa Rais Bashar al-Assad iwapo kutatokeza
ushahidi kwamba ulihusika na kile kinachoshukiwa kuwa ni shambulio la gesi ya
sumu ya klorini katika eneo linalodhibitiwa na waasi.
EMANUEL MACRON |
Aidha, Msemaji wa
serikali ya Ufaransa Benjamin Griveauksi ameiambia Redio Europe nambari moja,
kwamba taarifa za upelelezi za Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa na Donald Trump
wa Marekani zinaashiria silaha za kemikali zilitumika.
Hata hivyo, Viongozi
hao wawili wamezungumza kwa simu jana usiku kuhusu shambulizi lililotokea
kwenye mji wa Douma siku ya Jumamosi iliyopita ambapo zaidi ya watu 40 waliuawa
katika kile kinachotajwa kuwa ni shambulio la gesi ya sumu.
UFARANSA KULIPIZA KISASI
Reviewed by safina radio
on
April 11, 2018
Rating:
No comments