AMISOM YAITAKA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUISADIA SOMALIA


Tume ya Umoja wa Afrika ya Kulinda Amani nchini Somalia AMISOM imeitaka jumuiya ya kimataifa kusaidia Somalia kuijengea uwezo wa kukabiliana na vitisho nchini humo.

Image result for PICHA YA SOMALIA


Wakihitimisha mkutano wa nne wa mwaka, Maafisa wakuu wa AMISOM wakiwemo maafisa wa usalama wamefikia makubaliano juu ya hatua za kukabiliana kwa ufanisi na tishio la mabomu ya kienyeji linalozuia mchakato wa kupata utulivu nchini humo.

Mwakilishi maalum wa mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia Francisco Madeira, amewapongeza washirika mbalimbali kwa kuendelea kuwaunga mkono na kujitolea askari wake kwa AMISOM kukabiliana na tishio la mabomu ya kienyeji (IED) kwa vikosi vya usalama na raia wa Somalia.

Mapema mwezi huu Kitengo cha Huduma za kutegua Mabomu cha Umoja wa Mataifa kimesema kuwa takriban watu 3,000 wanasadikika kuuawa na kujeruhiwa kutokana na mabomu hayo nchini Somalia.

AMISOM YAITAKA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUISADIA SOMALIA AMISOM YAITAKA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUISADIA SOMALIA Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.