MAHAKIMU 250 WAFUTWA KAZI NCHINI DRC


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewafuta kazi Mahakimu 250 ambao hawana elimu ya sheria pamoja na wale ambao walikuwa wameshtumiwa kuwa mafisadi.

Image result for NEMBO YA MAHAKAMA YA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO DRC


Waziri wa Sheria wa nchi hiyo Alexis Thambwe Mwamba amesema hatua hii imechukuliwa ili kuwazuia watu waliokuwa wanaingia katika idara ya Mahakama wakiwa na lengo la kujipatia fedha badala ya kuwatumikia raia wa nchi hiyo.

Hii sio mara ya kwanza kwa serikali ya Kinshasa kuwachukulia hatua maafisa wa juu wa idara ya Mahakama kwani Mwaka 2009, rais Joseph Kabila aliwafuta kazi Majaji 96 baada ya kubainika kuwa walikuwa mafisadi.

MAHAKIMU 250 WAFUTWA KAZI NCHINI DRC MAHAKIMU 250 WAFUTWA KAZI NCHINI DRC Reviewed by safina radio on April 17, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.