TANGA KUJENGA SOKO KUBWA LA MATUNDA


Mkoa wa Tanga umejipanga Kujenga soko la Kimataifa la matunda na mboga mboga katika eneo la Segera Wilayani Handeni ili kuwa na uhakika wa kuuza bidhaa za mashambani na kupata bei nzuri ya ushindani.

Image result for PICHA YA SOKO LA KISASA LA MATUNDA

Hayo yamesemwa na katibu tawala wa Mkoa huo  Bi,Anuciata Lyimo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na namna ambavyo wamejipanga kuimarisha hali ya masoko mkoani humo.

Amesema kuwa ili wakulima wa matunda waweze kupata soko la uhakika mkoa huo unadhamiria kujenga soko la kimataifa katika eneo la Segera ili kuwawezesha wakulima kunufaika na bei nzuri za bidhaa wanazozizalisha wenyewe mashambani.

Pia  ameongeza kuwa ili kuhakikisha wakulima wananufaika na soko lenye tija mkoa  huo umejikita kuboresha masoko yote  ya ndani kwa kuweka miundombinu ya maji ,vyoo,umeme,na barabara ili kuhakikisha kwamba bidhaa zinazozalishwa zinapata soko la uhakika ndani na nje ya nchi.

Aidha Bi Lyimo ameelezea changamoto inayoikabili sekta ya masoko mkoani humo kuwa ni kukosekana kwa soko la uhakika kwa bidhaa zinazozalishwa viwandani kutokana na matumizi ya vifungashio duni pamoja na ukosefu wa mitaji mikubwa ya kufufua na kuendeleza viwandwa vilivojengwa miaka ya 1980.


TANGA KUJENGA SOKO KUBWA LA MATUNDA TANGA KUJENGA SOKO KUBWA LA MATUNDA Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.